Meneja Mradi wa Taasisi ya Sekta Binafsi (TPSF) Celestine Mkama (kushoto) ) akizungumza kwenye Mkutano na waandishi wa habari Dar es salaam, kuhusu mafunzo yatakayotolewa kwa wajasiriamali wadogo na wa kati kupitia tovuti ya taasisi hiyo. Katikati ni Mkurugenzi Mtendaji Mkuu wa Taasisi hiyo, Godfrey Simbeye na Mtaalamu wa ujasiriamali na maendeleo ya kiuchumi, Haji Dachi. Mkurugenzi Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Sekta Binafsi (TPSF),Godfrey Simbeye (katikati) akizungumza kwenye Mkutano na waandishi wa habari Jijini Dar es Salaam, kuhusu mafunzo yatakayo tolewa kwa wajasiriamali wadogo na wakati kupitia tovuti ya taasisi hiyo. Meneja mradi wa TPSF Celestine Mkama (kushoto) wa mwisho kulia Mtaalamu wa ujasiriamali na maendeleo ya kiuchumi, Haji Dachi.
Mtaalamu
wa ujasiriamali na maendeleo ya kiuchumi, Haji Dachi (kulia)
akizungumza na waandishi wa habari Dar es salaam, namna wajasirimali
wadogo na wakati watakavyo weza kunufaika na mafunzo yatakayotolewa na
Taasisi ya Sekta Binafsi (TPSF) kupitia tovuti ya Taasisi hiyo . kushoto
ni Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi hiyo, Godfrey Simbeye.
Taasisi
ya Sekta Binafsi Tanzania (TPSF) kwa kushirikiana na Mfuko wa
Kuendeleza Sekta ya Fedha Tanzania (FSDT) itaendesha mafunzo maalum kwa
wajasiriamali nchi nzima kuhusu namna ya kunufaika na tovuti mpya ya
habari kwa wajasiriamali.
Akiongea
kwenye mkutano na waandishi wa habari jijini Dar es salaam leo,
Mkurugenzi Mkuu wa TPSF, Godfrey Simbeye amesema taasisi hiyo imeanzisha
vipindi vya redio katika vituo mbalimbali vya redio za kitaifa na vituo
vidogo vya redio za jamii katika mikoa ya Dodoma, Geita, Kigoma na
Mbeya. Vipindi hivyo vya redio vitaenda sambamba na warsha za mafunzo
zitakazowahusisha wajasiriamali na wadau mbalimbali katika mikoa hiyo.
“Kampeni
hii imelenga kuongeza uelewa wa wajasiriamali juu ya tovuti hiyo ambayo
ina mifumo ya mafunzo kwa wajasiriamali, namna ya kuanzisha na kukuza
biashara, upatikanaji wa mitaji, mbinu sahihi za kuendesha biashara,
namna ya kutafuta na kuuza bidhaa katika masoko, vilevile kampeni itatoa
jukwaa la majadiliano kuhusu mada mbalimbali zinazowahusu wajasiriamali
wadogo nchini.” alisema Simbeye.
Mafunzo
yatatolewa nchi nzima na wataalamu waliobobea katika biashara na
ujasiriamali kwa kipindi cha miezi nane ili kuwajengea uwezo
wajasiriamali waweze kunufaika ipasavyo na tovuti hiyo iliyozinduliwa
mapema mwaka huu na Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles
Mwijage mapema mwaka huu. Tovuti hiyo inayopatikana kupitia
www.entrepreneurs.or.tz, www.wajasiriamalitz.or.tz au kwa kupiga namba
*148*99*06# ni kituo maalum chenye taarifa zote sahihi zinazomtosheleza
mjasiriamali kuendesha biashara kwa mafanikio.
“Huduma
hii imetolewa ili kuwasaidia wajasiriamali ili waweze kupata nyenzo
muhimu za kuendesha biashara, vyanzo vya fedha, kuingia kwenye masoko ya
hapa nchini na kimataifa, na taarifa nyingi za kuweza kumsaidia mtu
anayetaka kuanzisha biashara na kuwawezesha wale ambao tayari wanafanya
biashara kujiongezea ujuzi na uzoefu,” alisema Simbeye.
Meneja
Mradi wa Tovuti hiyo, Celestine Mkama alisema “Tumeona umuhimu wa
kuendesha kampeni ya kuongeza uelewa wa tangu wakati tunatengeneza mfumo
huu wa habari. Tunatarajia kupitia kampeni hii kuweza kuwafikia
wajasiriamali moja kwa moja kupitia vipindi vya redio na warsha na
kuweza kutatua matatizo yao kwa kuwapatia ujuzi”.
Hivi
sasa kuna wajasiriamali zaidi ya milioni tatu nchini na tunajua kwamba
ujuzi hafifu ni kikwazo kikubwa katika ukuaji wa biashara ndogo ndogo
ambazo ni muhimu sana katika ukuaji uchumi,” alisema Mkama. “Tunataka
kuhamasisha matumizi ya tovuti hii na kutoa mafunzo wakati huo huo.
Tunaamini jambo hili litawajengea uwezo na kuwapa wajasiriamali ujuzi
muhimu wa kuendesha biashara endelevu.”
No comments:
Post a Comment