JIACHIE

Karibuni Jamvini Wanajamii

Tangaza Hapa

Post Top Ad


UTIAJI SAINI MAKUBALIANO YA AWALI YA UJENZI WA RELI YA KATI (STANDARD GAUGE)

Share This
 Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango Dkt. Servaciaus Likwelile akitiliana saini na Naibu Meneja Mikopo Nafuu wa Benki ya Exim ya China Bw. Zhu Ying kuhusu makubaliano ya awali ya ujenzi wa reli ya kati kwa kiwango cha kisasa (Standard Gauge), jijini Dar es Salaam.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango Dkt. Servaciaus Likwelile akibadilishana hati ya makubaliano na Naibu Meneja Mikopo Nafuu wa Benki ya Exim ya China Bw. Zhu Ying mara baada ya kusaini makubaliano ya awali ya ujenzi wa reli ya kati kwa kiwango cha kisasa (Standard Gauge), jijini Dar es Salaam.
Imetolewa na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano.

SERIKALI ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania leo imetiliana saini na Benki ya Exim ya China makubaliano ya awali ya ujenzi wa reli ya kati kwa kiwango cha kisasa (Standard Gauge).

Makubaliano hayo ya awali yamefanywa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango Dkt. Servaciaus Likwelile kwa niaba ya Tanzania na Naibu Meneja Mikopo Nafuu wa Benki ya Exim ya China Bw. Zhu Ying.

Akizungumza katika hafla hiyo ya utiliaji saini Dkt. Likwelile amesema hatua hiyo inawezesha hatua za upembuzi yakinifu, usanifu na uundwaji wa timu za pamoja kuanza kuanisha mahitaji halisi ya ujenzi wa mradi huo.

Zaidi ya Shilingi Trilioni 16 za Tanzania zinatarajiwa kutumika katika ujenzi wa mradi wa reli ya kati yenye urefu wa Kilometa 2,190 ambapo Benki hiyo itashirikiana na Serikali ya Tanzania katika ujenzi wake.

Mradi wa ujenzi wa reli ya kati utahusisha ujenzi wa reli kwa kiwango cha kisasa kutoka Dar es Salaam-Tabora-Isaka-Mwanza na Tabora-Mpanda-Kalemela-Uvinza-Kigoma-Isaka-Keza hadi Msongati.

Imetolewa na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad