Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na wazee, wafanyabiashara , viongozi wa dini na wanachi wa Dodoma kuhusu mikakati ya serikali ya kuhamia Dodoma kwenye ukumbi wa Hazina mjini Dodoma Julai 26, 2016. Wengine kutoka kushoto ni Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu, Uledi Mussa, Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, Anthony Mavunde na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Jordan Rugimbana.
Baadhi ya wazee, wafanyabiashara, viongozi wa dini na wananchi wa Dodoma wakimsikiliza Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa kuhusu mikakati ya serikali ya kuhamia Dodoma kwenye ukumbi wa Hazina mjini Dodoma Julai 26, 2016.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiwa katika picha ya pamoja na wazee wa Dodoma baada ya kuzungumza na wazee, viongozi wa dini, wafanyabiashara na wananchi wa Dodoma kwenye ukumbi wa Hazina mjini Dodoma Julai 26, 2016.
(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
No comments:
Post a Comment