JIACHIE

Karibuni Jamvini Wanajamii

Tangaza Hapa

Post Top Ad


MBUNGE COSATO CHUMI KUTATUA TATIZO LA MAJI KATIKA MJI WA MAFINGA LILODUMU KWA MUDA MREFU.

Share This

Mbunge wa mafinga mjini cosato chumi akikagua chanzo maji cha ikangafu wakati wa ziara yake ya kutembelea vyanzo vya maji na matanki ya kuhifadhia maji

Mbunge wa mafinga mjini cosato chumi akikagua moja ya tanki la kuhifadhia maji.
kushoto ni bw uhaula ,bw shaibu nnunduma mkurugenzi wa halmashauri ya mji wa mafinga wakijadili jambo baada ya kukagua baadi ya vyanzo hivyo vya maji.

MBUNGE wa jimbo la mafinga mjini cosato chumi amefanya ziara ya kuangalia jinsi gani anaweza kutatua tatizo la maji katika jimbo hilo.leo mapema mbunge huyo aliongozana na wataalamu wa maji na mkurugenzi wa maji wa mafinga walifanya ziara kwenye vyanzo vya maji kwa lengo la kutatua tatizo la maji ambalo limedumu kwa kipindi kilefu.

Akizungumza katika ziara hiyo chumi amesema kuwa ameamua kufanya ziara katika eneo hilo kwa lengo la kujua nini tatizo linalosababisha miji wa mafinga kuwa na uhaba wa maji."huwezi kutatua tatizo bila kulijua tatizo lenyewe hivyo nimelazimika kufanya ziara na kufika huku ili nijionee mwenye nini tatizo na nianze kuangalia na kupanga mikakati ya kulitatua tatizo hilo ambalo limekuwa sugu katika mji huo" alisema chumi.

aidha mh chumi alisema kuwa mji wa mafinga unahitaji maendeleo hivyo moja ya mambo yanayosababisha maendeleo ni maji hivyo ni lazima kulitatua tatizo hilo mapema ili wananchi waendelee kufanya kazi na kuacha kulifikilia tatizo hilo ambalo limekuwa likiwagharimu muda mwingi wa kwenda kutafuta maji. 

"leo nimekuja na wataalamu wa maji wa mji wa mafinga ili wanieleze nini tatizo kitaalamu na tutumie njia gani kulitatua tatizo hilo ndio maana unaniona nipo na hawa wataalm lengo langu ni kulimaliza kabisa tatizo la maji katika mji huu wa mafinga" alisema chumi.

pia chumi amewahakikishia wananchi wa jimbo la mafinga mjini kuwa atahakikisha anatatua tatizo hilo kwa kuwa ili kuwa moja ya sera yake wakati wa kuomba kura kwa wananchi hivyo lazima atimize ahadi aliyoihaidi.

chumi amemalizia kwa kuwaomba wananchi wa jimbo hilo kumpa ushirikiano kwa jambo lolote lile analolifanya la maendeleo katika jimbo hilo na kuwaomba wawe na subira wakati anapanga mikakati ya kutengeleza ahadi zake alizozitoa wakati wa kuomba kura.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad