2015-09-28
Jumuiya ya Watanzania Sweden
Mahali: Näsby Alle´6
183 55 Näsby Park
Siku: Jumamosi
Tarehe: 31-10-2015
Saa: 9:00 jioni
Kwa watanzania tunatoa taarifa ya wito wa Mkutano Mkuu wa ziada kwa
ajili ya kuchagua viongozi watakao chukua majukumu ya kuwaongoza watanzania
waishio nchini Sweden, na kujenga uhusiano na taasisi mabali mbali na vyama
vyengine viliopo nchi jirani.
Uongozi wa kamati ya maandalizi ya Jumuiya ya Watanzania inawataarifu
kwamba nafasi za uongozi huo ni kama zifuatazo;
Uenyekiti
Unaibu
Ukatibu pamoja na bodi ya utawala wa
chama.
Tunawaomba watanzania wajutokeze kwa wingi katika mkutano huo ili tuweze
kuboresha umoja wetu na kujenga maadili bora kwa watanzania, kujitolea kwenu
ndio mafanikio ya taifa letu.
Asanteni
Kamati ya matayarisho
No comments:
Post a Comment