JIACHIE

Karibuni Jamvini Wanajamii

Tangaza Hapa

Post Top Ad


GENERAL MOTORS WARUDI KWA KISHINDO

Share This
 Mwenyekiti wa QAML Mwenyekiti,Yusuf Manji wa kwanza kulia, Rais na Mkurugenzi Mtendaji wa  Kampuni ya magari ya General Motors East Africa (GMEA) Limited, Mario Spangenberg wakikata utepe kuashiria uzinduzi wa jengo la Isuzu uzinduzi huo uliofanyika jiji Dar es Salaam leo.
Mkurugenzi mtendaji wa Kampuni ya General motors (GMEA) Bi. Rita Kavashe  akisaini makubaliano ya kibiashara na Mwenyekiti Mtendaji wa Kampuni ya Quality automotive Vinay Upadhyay.
 Mkurugenzi mtendaji wa GMEA Rita Kavashe alisema Kampuni ya General motors kuingia katika soko la Tanzania ilikuwa ni sehemu ya mkakati wa muda mrefu katika kampuni hiyo ili kuimarisha uwepo wake Afrika Mashariki. Kulia ni Rais na Mkurungenzi Mtendaji wa (GM) Africa  Mario Spangenberg.


Wakifurahia jambo mara baada ya kukamilisha makubaliano.
PICHA NA EMMANUEL MASSAKA


General Motors Imerudi tena katika soko la Tanzania ikiwa imeongeza ufanisi zaidi, 

Wenya magari Tanzania leo wana sababu ya kutabasamu maana Kampuni ya magari ya General Motors East Africa (GMEA) Limited leo wamesaini makubaliano ya kibiashara na Quality automotive mechanization limited (QAML) ambayo itashuhudia  kampuni ya magari ikiingia kwenye soko la Tanzania.

Kupitia uuzaji mpya, wateja wa General Motors wataweza kununua bidhaa mpya aina ya Isuzu na Chevrolet kutoka katika sehemu za mauzo huku wakipata huduma za kimataifa kutoka katika eneo maalumu la magari hayo.

Akizungumza hi leo wakati wa sherehe ya kutia saini makubaliano ya biashara, Mwenyekiti Mheshimiwa wa QAML Mwenyekiti Mheshimiwa Yusuf Manji aliahidi wateja ngazi bora ya urahisi na faraja.

 “Tumeweka uwekezaji mkubwa/muhimu kuhakikisha mafanikio ya kituo hiki na kuwezesha kupenya kwa haraka kwa bidhaa za Isuzu na Chevrolet katika soko hili lenye ushindani mkubwa”.

 Alisema
Eneo la mauzo ya magari limetengenezwa ili kutoa/ kuwapatia wateja uzoefu na uimara kwa ujumla na bidhaa za General Motors, pamoja na kutoa huduma za mauzo na vifaa vya magari.

Mkurugenzi mtendaji wa GMEA Bi. Rita Kavashe alisema Kampuni ya General motors kuingia katika soko la Tanzania ilikuwa ni sehemu ya mkakati wa muda mrefu katika kampuni hiyo ili kuimarisha uwepo wake katika Afrika Mashariki.

“Tanzania imejitokeza katika soko na kama General Motors tulitaka kuwa sehemu ya ukuaji huu. Sehemu hii ya mauzo itakuwa ni hatua ya kuingia kwa bidhaa zetu zenye ubora na zimetumia utaalamu mkubwa katika utengenezwaji wake  ambapo tunatanua wigo wetu katika ukanda huu. Kupitia uuzaji huu, wateja wetu watanunua aina mpya za Chevrolet na Isuzu huku wakipata huduma bora”.

Alisema Bi. Kavashe alisema kuingia ndani ya soko la Tanzania imetokana na kukua kwa kasi kwa biashara ndani ya ukanda wa Afrika Mashariki hasa katika kuendeleza ushirikiano wa masoko ya umoja. Soko la jumuia ya Afrika Mashariki lina takribani watu milioni 140 .
“Tanzania ni soko linalokua kwa kiwango kikubwa na imekua ni soko muhimu tunalolitazamia tunapotafuta kujikita katika soko lenye watu wengi na idadi inayokua kila kukicha. Ukuaji wa viwanda na


kuongezeka kwa kipato ili kutengeneza ongezeko la watu wa tabaka la kati katika nchi hii ina maana kuwa kuna soko changa la bidhaa zetu, “aliongezea Kavashe.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad