Wednesday, July 18, 2012

SERIKALI ya Mapinduzi Zanzibar yakiri wazi ugonjwa wa kansa na kifafa ni tatizo

Na Khadija Khamis    - Maelezo     Zanzibar
                  18/07/2012.

SERIKALI ya Mapinduzi Zanzibar imesema kuwa ugonjwa wa kansa na kifafa ni miongoni mwa magonjwa sugu yanayowasumbua wananchi wa rika zote na kwa uhakika ni kwamba tatizo hilo halijapatiwa ufumbuzi ulimwenguni kote.

Akijibu suala la Mwakilishi  Mohammed Said Muhammed Jimbo la Mpendae  aliyetaka kujua hatua gani unayochukuliwa na Serikali ya kupata tiba ya maradhi  hayo pamoja na kufanya utafiti wa kina wa kuweza kujua asili na suluhisho la maradhi hayo  .

Naibu waziri wa Afya Dk Sira Ubwa  Mamboya alisema kuwa maradhi ya kansa na kifafa ni maradhi ya zamani na ni sugu ambayo yana sababu nyingi na zinazotofautiana . Alisema kuwa kwa hapa Zanzibar tuna madaktari ambao wanafanya kazi na kuchunguza na kuweza kutambua na wanapoweza kutoa tiba sahihi ya saratani na kifafa  wanatoa ipasavyo kwa wagonjwa wa maradhi hayo .

Aidha alisema kuwa kutokana na sababu nyingi zinazojitokeza kwa maradhi hayo hata nchi zilizoendelea huwa zinataratibu zake za kuwa na wataalamu maalum ambao wanashungulikia tafiti  tu za maradhi hayo na sababu nyingi za saratani na kifafa hazijaweza kujulikana vizuri hadi sasa “tatizo la maradhi hayo ni sugu na linachukuwa muda mrefu matibabu  yake  kila baada ya muda mgonjwa atahitaji kufanyiwa uchunguzi “alisema Dk Sira. 

Dk sira alisema matibabu ambayo yanatolewa katika hospitali kuu ya mnazimmoja ni yale tu yanayowezekana kufanyika yasiyoweza kufanyika hapa wagonjwa hao hupelekwa nchi za nje kwa matibabu zaidi . Naibu huyo alisema kuwa wagonjwa huwa wanasafirishwa nchi za nje kutokana na kukosekana mashine za vipimo vya maradhi hayo serikali husafirisha wagonjwa hao kwa kufanyiwa matibabu lakini kuna baadhi ya wagonjwa ambao wanakuwa na haraka ya matibabu huamua kujigharamia wao  wenyewe . Aidha alieleza kuwa wizara ya afya imeweza kufungua  kitengo maalum  ambacho kimetekwa kwa maradhi hayo ambayo yanaonekana ni sugu  na ya muda mrefu .

Kuna Maoni 0 mpaka sasa.