Taarifa zilizotufikia hivi punde ni kwamba meli ya abiria ya Stargic inayomilikiwa na kampuni ya Seagul iliyokuwa ikielekea visiwani Zanzibar ikitokea Dar es Salaam imezama muda huu. Meli hiyo ilitoka Dar es Salaam leo saa 7 mchana ikiwa na abiria karibia 200 na kuzama katika eneo la Chumbe jirani na Zanzibar. Mpaka sasa haijafahamika madhara yaliyotokana na ajali hiyo.Mtandao wako utazidi kukupa habari zaidi kuhusiana na tukio hili.




Kuna Maoni 0 mpaka sasa.
Post a Comment