Sunday, January 29, 2012

NAFASI ZA KAZI YA UWAKALA WA USAMBAZAJI VITABU

NAFASI  ZA  KAZI

Mambo  PUBLISHERS  ni  wachapishaji  na  wauzaji  wa  vitabu  mbalimbali  vya  ziada   na  kiada.
Tunatangaza  nafasi  za  kazi  ya    uwakala   wa  usambazaji  vitabu  vyetu   kwa  wateja  wetu  waliopo  katika    maeneo  mbalimbali  nchini  Tanzania

SIFA  ZA  MWOMBAJI  NAFASI.
1.       Umri  miaka  18  hadi 45.   2.   Elimu  kidato  cha  nne , cha  sita  na  kuendelea.
2.       Awe  smart ( maridadi  )  na  anayejituma  kazini.
3.       Awe  tayari  kufanya  kazi  katika  kituo  chochote  cha  kazi  atakacho  pangiwa kilichopo  ndani  ya  wilaya  anayo  ishi.
4.       Awe  na  uwezo  wa  kununua   kwa  bei  ya  jumla  kuanzia  vitabu  kumi  na  kuendelea  kwa  ajili  ya  kuvisambaza  kwa  wateja  wetu  mbalimbali  waliopo  katika  eneo   ama  kituo  atakacho  pangiwa.
5.       Awe   na  uwezo  wa  kuandika  na  kuongea  kwa  ufasaha  lugha  za  Kiswahili  na  kiingereza.
6.       Akiwa  na  uzoefu  wa  kazi  ya  usambazaji    vitabu, magazeti, majarida  au  bidhaa  yoyote  ile, itakuwa  ni  sifa  ya  ziada  itakayo  muongezea  nafasi  ya  kupata  kazi  hii.

MAJUKUMU  YA  KAZI
Kwa  mwombaji  atakaye  pata  nafasi  hii  ya  kazi  atakuwa  na  majukumu  yafuatayo :
Kununua   vitabu  kutoka  ofisini  kwetu,  kiwandani  au  kwa  wakala  wetu   kwa  bei  ya  jumla  na  kuvisambaza  kwa  wateja  wetu   waliopo  katika   maeneo  yaliyo  karibu  na  kituo  chake  cha  kazi.

Tuma   barua  yako  ya  maombi  ya  ukiambatanisha  na  C.V  yako kwenda  kwa :
Managing  Director  ,
Mambo  PUBLISHERS
S.L.P  35967
Dar  es  salaam 
Au  tuma  maombi  yako  kupitia  barua   pepe  yetu : mambopublishers@gmail.com.
TUNAPOKEA  MAOMBI  KUTOKA  KWA  WAOMBAJI    KUTOKA  KATIKA  WILAYA  ZOTE  ZA  TANZANIA  BARA  NA  VISIWANI.

Mwisho  wa  kupokea  maombi  ni  tarehe  05 FEBRUARI  2012   , kazi  kuanza  tarehe  13 FEBRUARI 2012. Watakao   timiza  vigezo  vya  maombi  ndio  watakao  itwa  ofisini  kwa  ajili  ya  usaili.

Kuna Maoni 0 mpaka sasa.