wasanii wa fiesta jipanguse 2010,kupitia kampeni ya zinduka watoa msaada wa vyandarua hospitali ya Sekou Toure jijini Mwanza.

Saturday, July 31, 2010
Shoto ni B Dozen,Young D,Rebeca kutoka kituo cha THT,Mwasiti pamoja na waja wazito katika picha ya pamoja jioni hii,mara baada ya kuwakabidhi Vyandarua vya msaada kupitia mpango mzima wa kampeni ya kupambana na malaria nchini wa ZINDUKA.
Mabalozi wa Malaria nchini wakiwa wamepozi picha ya pamoja na waja wazito jioni hii mara baada ya kuwakabidhi Vyandarua vya msaada kupitia mpango mzima wa kampeni ya kupambana na malaria nchini wa ZINDUKA.
Mtangazaji wa Clouds FM B dozen kwa niaba ya wasanii wenzake akizungumza machache mbele ya Wazazi ndani ya wodi ya wazazi ndani ya hospitali ya mkoa wa Mwanza, Sekou Toure mara baada ya kuwakabidhi vyandarua leo jioni ,yote hiyo ikiwa ni kwenye mpango mzima wa kampeni ya kupambana na ugonjwa wa malaria iliyozinduliwa hivi karibuni ya ZINDUKA.
Mtangazaji wa Clouds FM Hamis Mand a.k.a B Dozen akiwakabidhi Vyandarua Muuguzi mkuu (kushoto) Bi.Eva Mudayi pamoja na afisa muuguzi wa wodi hiyo Bi Adelina jioni hii,yote hiyo ikiwa ni kampeni ya kupambana na ugonjwa wa Malaria kupitia mpango wa ZINDUKA.
Wasanii wa muziki wa kizazi kipya ambao wapo kwenye ziara ya tamasha la Fiesta Jipanguse 2010,ambao pia ni mabalozi wa Malaria hapa nchini,Mwasiti pamoja na Chege wakiwakabidhi Vyandarua Muuguzi mkuu (kushoto) Bi.Eva Mudayi pamoja na afisa muuguzi wa wodi hiyo Bi Adelina jioni hii,yote hiyo ikiwa ni kampeni ya kupambana na ugonjwa wa Malaria kupitia mpango wa ZINDUKA.

Pichani kulia ni Muuguzi mkuu Bi.Eva Mudayi akitoa muongozo wa awali kwa baadhi ya wasanii nje ya Wodi ya Wazazi kabla ya kukabidhi msaada wa Vyandarua jioni ya leo ndani ya hospitali ya mkoa wa Mwanza ya Sekou Toure.
Pichani kulia ni Muuguzi mkuu Bi.Eva Mudayi akiwaongoza baadhi ya wasanii wa muziki wa kizazi kipya kwenda kukabidhi msaada wa vyandarua kwenye wodi ya Wazazi jioni hii.Mbele kabisa ni wasanii Godzilla na Chege wakiwa wamebeba vyandarua.
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Saturday, July 31, 2010 | | Permalink | Maoni 0

dr slaa azidi kufunika,wakazi wa jiji la mwanza na mara wampokea kwa shangwe

Mwanachama wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mabere Marando, ambaye alijunga na chama hicho hivi karibuni akitokea chama cha NCCR Mageuzi, akiwahutubia wakazi wa jiji la Mwanza, katika mkutano wa hadhara wa kuomba kudhaminiwa, aliuofanyika kwenye Uwanja wa Furahisha jana
Mwenyekiti wa CHADEMA akiwatambulisha wakazi mjini Mwanza.
Mgombea urais kwa tiketi ya Chama cha Deokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Wilbrod Slaa, akilakiwa na wakazi wa mji wa Musoma, mara baada ya kuwasili kwenye Uwanja wa ndege wa Musoma, akitoea Arusha jana, ambako alikwenda kuomba udhamini.
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Saturday, July 31, 2010 | | Permalink | Maoni 1

laptop zinauzwa.

Nauza Laptop Mbili zilizotumika kidogo na ziko katika hali nzuri sana. Zina sifa zifuatazo:

Ya kwanza ni HP DV2054, Intel Core Duo, 2GB RAM, 250GB HD, DVD RW, Win XP Home, 14inch LCD, 3Hrs Battery Bei yake ni Tshs 800,000 tu.

Na ya pili ni DELL Inspiron 1505, Intel Core Duo, 3GB Ram, 160GB HD, Win Vista Home, 15 Inch LCD, DVD RW, hii inauzwa Tshs 750,000 tu.

Mteja mwenye nia anipigie simu 0713458746.

Siku na kazi njema.
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Saturday, July 31, 2010 | | Permalink | Maoni 0

rais karume apiga kura ya maoni zanzibar leo

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk Amani Abeid
Karume,akitumbukiza kura yake,katika kituo cha kupigia kura ya Maoni, ya kuwezesha Uundwaji Serikali ya Kitaifa ya Zanzibar,katika Skuli ya Msingi ya Kiembesamaki Wilaya Magharibi jana,Uundwaji wa Serikali hiyo ya Kitaifa ni baada ya Uchaguzi Mkuu ujao wa mwezi Octoba mwaka 2010.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk Amani Abeid
Karume,akikabidhi kitambulisho cha upigaji wa kura kwa karani No 1 Asha Mustafa Abdalla,katika kituo cha upigaji wa kura ya maoni cha Skuli ya Msingi Kiembesamaki leo.Picha na Ramadhan Othman Ikulu,Zanzibar.

 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Saturday, July 31, 2010 | | Permalink | Maoni 0

karne ya 21 ndani ya jiji la dar.!

Wanafunzi wa Darasa la saba wa Shule ya Msingi Mtoni Jijini Dar es Salaam, wakiwa katika masomo yao ya kila siku nje ya madarasani chini miti wakati wakifundishwa na mwalimu wao leo mchana.

Walimu wa shule hiyo baada ya kuona kamera ya Sufianimafoto ikiwa kazini walijitetea kuwa wameamua kuwakusanya wanafunzi hao wa mikondo minne na kuwafundisha kwa pamoja, ili waweze kuelewa kwa pamoja kuelekea kujiandaa na mitihani ya darasa la saba ya mwaka huu. Lakini cha kushangaza ni kwamba kama hivyo ndivyo imekuwaje wanafunzi hao wote wafundishwe na mwalimu mmoja je wataweza kuelewa na lengo lao litatimia kweli?

MATATIZO YA OFISI ZA WALIMU BADO NI CHANAGAMOTO..!!!

Walimu wa Shule ya Msingi Twiga ya Jijini Dar es Salaam, wakisahihisha madaftari ya wanafunzi wao wakiwa chini ya miti nje ya madarasa jambo linaloonyesha kuwa shuleni hapo kunaupungufu wa madarsa na ofisi za walimu.

MADARASA KAMA HAYA KWELI WANAFUNZI WATASOMA KWA BIDII?

Hili pia ni moja kati ya madarasa ya Shule ya Msingi Twiga, kwakweli yanakatisha tamaa kwa wanafunzi kujisomea kwa bidii na hata kwa mzazi anayefika shuleni hapo na kuona mazingira hayo. Hapa mvua ikinyesha ni balaa na naamini ndani ya darasa hili patakuwa hapakaliki, Wadau hebu liangalieni hili kwa macho manne ili tukomboe Elimu ya Tanzania kwani hapa ni ndani ya Jiji kubwa na lenye maendeleo mengi na kila kitu kizuri na zaidi Jiji hili ndilo hasa lenye ofisi za wakuu wote wa nchi hii Je wakuu mnaridhika kweli kuwa na madarasa kama haya katika jiji kama hili? Kama Dar tu ni hivi je Vijijini ni vipi????

Wanafunzi hao wakiendelea kufundishwa na hapa wamepigwa kwa nyuma ili kuonyesha uhalisia wa mahala penyewe na uwingi wao ambao bado wamekatwa kulingana na kamera kwa kweli ni wengi mno.Picha zote kwa hisani ya www.sufianimafoto.blogspot.com

 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Saturday, July 31, 2010 | | Permalink | Maoni 1

Watatu watuhumiwa na shambulio la Uganda

Watuhumiwa wa shambulio la Uganda

Wakenya watatu wameshtakiwa kwa mauaji ya watu 76 waliouliwa wakati mabomu yalipolipuka walipokuwa wakitazama fainali ya Kombe la Dunia kupitia televisheni mjini Kampala, Uganda.

Hussein Hassan Agad, mwenye umri wa miaka 27, Mohamed Adan Abdow, 25 na Idris Magondu, 42, nao walishtakiwa kwa ugaidi na mashtaka 10 ya jaribio la mauaji.

Bado hawajajitetea na wataendelea kubaki kizuizini mpaka wafikishwe tena mahakamani Agosti 27.Al-Shabab, kundi la wapiganaji la kisomali, lilisema lilihusika na mashambulio hayo.

Majeshi ya kutunza amani ya Uganda yapo Somalia, kusaidia serikali dhaifu, inayoungwa mkono na umoja wa mataifa dhidi ya al-Shabab, yenye uhusiano na al-Qaeda.

Umoja wa Afrika wiki hii iliahidi kuongeza majeshi ya kutunza amani Somalia kufikia majeshi 4,000, baada ya mkutano uliofanyika Kampala, mji uliokumbwa na mashambulio.

Mpaka sasa ni Uganda na Burundi tu ndizo zilizopeleka majeshi yake katika mji mkuu wa Somalia, Mogadishu na al-Shabab ilitishia kushambulia nchi zote mbili.Chanzo BBC.

 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Saturday, July 31, 2010 | | Permalink | Maoni 0

shoo love kwa hisani ya serengeti,kinywaaji maalum cha fiesta jipanguse 2010

Msanii Diamond akiwa amepozi na densa wake kabla ya kupanda jukwaani.
Vichwa makini kutoka Clouds FM;Mull B,Ncha Kali na Dj Fetty
Mmechisho safi kabisa wa Mfalme wa raha kamili
Kutoka kushoto ni G wala wala,B Dozen,Joe Makini na Nick Mbishi wa Pili
Mdau akiwa amepozi Wafamle wa raha kamili
Msanii Roma (nyeupe) akiwa amepozi na mashabiki wake kwa picha.
Amin,Lina pamoja na Mwasiti katika pozi la picha kabla ya kupanda jukwaani usiku wa kuamkia leo katika tamasha la Fiesta jipanguse lililofanyika ndani ya Musoma Hotel,na leo tamsha la Fiesta linahamia jijin Mwanza ambapo linafanyika Usiku ndani ya Yatch Club na kesho Uwanja wa CCM Kirumba.
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Saturday, July 31, 2010 | | Permalink | Maoni 0

maelfu ya wakazi wa musoma wajitokeza tamasha la fiesta jipangusa 2010.

Msanii wa hipo hop anaekuja kwa kasi katila anga ya muziki wa Bongofleva anaetamba na nyimbo zake kadhaa ukiwemo wa Mr President,Roma akikamua jukwaani usiku wa kuamkia leo katika tamasha la Fiesta Jipanguse 2010 ndani ya Musoma Hotel,Roma ni msanii ambaye kwa kiasi kikubwa amewakuna vilivyo wakazi wa Musoma kutokana na mashairi yake yenye ujumbe wa kutosha.
Umati wa watu ulivyofurika ndani ya Musoma Hotel usiku wa kuamkia leo.
Wasanii wa kundi la TMK Wanaume Halisi likiongozwa na Juma Nature wakilishambulia jukwaa kwa kasi.
Wasanii Chege na Mh Temba wote kutoka kundi la Wanaume TMK wakikamua jukwaani,huku washabiki wao wakiweka mikono juu kuashiria kukunwa vyema na nyimbo zao.
Farid Kubanda a.k.aNgosha akishusha mistari ya nguvu mbele ya umati mkubwa wa wakazi wa Musoma waliojitokeza kwa wingi kwenye tamasha la Fiesta Jipanguse 2010,ambapo mdhamini wake mkuu ni kampuni ya Bia ya Serengeti.
Anajiita Mwamba wa Kaskazini,Joe Makini jukwaani.
Msanii Hussein Machozi akiwambia wakazi wa Musoma waliojitokeza kwa wingi kwenye tamasha la Fiesta Jipanguse 2010.
Mkali wa Moro Bell 9 akiwaimbia wakazi wa Musoma wimbo wake wa Masogange uliowavutia washabiki wake,usiku wa kuamkia leo ndani ya Musoma Hotel.
Wakazi wa Musoma walikuwa live ile mbaya,full kujipangusa kila wakati huku mfalme wa raha kamili akipewa nafasi yaka kama kawaida.
Msanii chipukizi mahiri katika muziki wa anga ya bongfleva ,Diamond akiimba wimbo wake wa Mbagala kwa wakazi wa Musoma usiku wa kuamkia leo ndani ya tamasha la Fiesta Jipanguse 2010.
Diamond akiwa amebebwa juu na mashabiki wake huku akiwaimbia mpango mzima wa Mbagala
Mkali mwingine wa hip hop bongo ,Godzilla kutoka Sala sala a.k.a Broklyn akiangusha mitindo huru kwa wakazi wa Musoma usiku wa kuamkia leo ndani ya musoma hotel,ambapo maelfu ya watu walijitokeza kujipangusa.
Wakazi wa Musoma wafunikana kwa kujipangusa,bila kucheza mbali na mfalme wa raha kamili
Msanii mahiri ambaye amekuwa akifanya vyema kwenye ziara hii ya tamasha la Fiesta Jipanguse,Mwasiti akiwarusha mashabiki wake na wimbo anaotamba nao kwa sasa uitwao kisa pombe.
Full rrrhhhhaaaa kila mahali
Msanii Mataluma kutoka THT akionesha umahiri wake wa kucheza na kuimba jukwaani.
Washabiki wakiserebuka taratiibu.
Wakali wa Bata kutoka Zenj,Offside Trick wakiwarusha bata wao jukwaani kwa pamoja nao bila hiyana aah ni kujiachia tu kwa kwenda mbele huku mfalme wa raha kamili akiwa tayari amekita mahali pake.
Kutoka nyumba ya vipaji THT,Barnaba na Lina wakiimba wimbo wao wa Kisa meseji ambao umeonekana kukubalika vyema kabisa kwa washabiki wao.
Lina akimpagawisha shabiki wake jukwaani
Wakazi wa Musoma walivyojitokeza kwa wingi ndani ya Musoma hotel usiku wa kuamkia leo kwenye tamasha la Fiesta jipanguse 2010,tamasha hilo mdhamini wake mkuu ni kampuni ya bia ya Serengeti.
Wasanii wenye vipaji vya kuimba kutoka THT,Amin na Barnaba wakiimba wimbo wao wa Robo saa.
Mfalme wa raha kamili tayari amedumisha raha zaid kwa washabiki hawa,ambpo mmoja wao alijifanya Chui Chui.
Msanii aliyewahi kufanya vyema katika shindano la Bongo Star Search,kutoka Mwanza,Beatrice akikamua hip hop lwa staili ya kipekee kabisa iliowavutia washabiki waliofurika ndani ya Musoma Hotel usiku wa kuamkia leo.
Kijana mdogo lakini mambo yake ni makubwa,anajiita Young D a.k.a Young Millionea akikamua jukwaani.
Ama kwa hakika wakazi wa Musoma bado wanazidi kuivunja historia yao ya kujitokeza kwa wingi kwenye matamasha ya Fiesta kila mwaka yanapofanyika,safari hii wamejitokeza kwa wingi na kuonekana live kushangweka kila wakati,huku wakiburudika na mfalme wa raha kamili,tamasha la fiesta Jipanguse mdhamini wake mkuu ni kampuni ya bia ya Serengeti kupitia vinywaji vyake mbalimbali ikiwemo Tusker,Uhuru bia,Villta Malt,Malta Guinnes na vinywaji vingine vikali.
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Saturday, July 31, 2010 | | Permalink | Maoni 0
Idadi ya watu