



Pichani ni baadhi ya wakazi wa Msasani wakisajili namba zao simu leo mchana kama walivyokutwa na Jiachie Utawala wa Urban Pulse unapenda kuwaletea exclussive behind the scenne kwa wadau wote wa libenekene kuhusu matayarisho na maandalizi ya Miss & Mr East Africa Uk 2010 yaliyofanyika katika kitongoji cha Edmonton, Ukerewe jumamosi 26.6.10
Fainali ya kuwania Taji la U Miss na U Mr East Africa UK litafanyika Jumamosi Julai 3, 2010 katika ukumbi wa Central Hall,Westminister, London


Hadi sasa Raila Odinga mwenye umri wa miaka 65 amekuwa ni mtu mwenye nguvu.
Katika miezi ya hivi karibuni amekuwa akipigia debe katiba mpya inayopendekezwa na hajaripotiwa kuwa na matatizo ya kimwili.
Kwa hiyo taarifa iliyotolewa hii leo na msemaji wake imewashangaza wengi.
Kwa mujibu wa taarifa hiyo madaktari wameamuru Odinga alazwe hospitalini kwa muda wakisema tu kwamba ana uchovu. Cha kukanganya ni kwamba taarifa hiyo iliwanukuu madaktari hao pia wakisema Odinga ana uwezo wa kufanya kazi kama kawaida ikiwa atajisikia kufanya hivyo. Japo hawatamruhusu kufanya hivyo.
Hadi sasa, maswali mengi kuhusu afya ya kiongozi nchini Kenya yameelekezwa kwa Rais Mwai kibaki ambaye baada ya uchaguzi wa mwaka 2003 kulikuwa na tetesi kwamba alipata kiarusi.
Hata hivyo maafisa wake walikanusha madai hayo wakisema alikuwa na matatizo madogo tu ya kiafya.
Msanii Vumi akielezea ujio wake mpya katika anga ya muziki wa kizazi kipya a.k.a bongofleva.Vumi anasema hivi sasa yuko kwenye harakati za kuikamilisha albamu yake itakayokuwa na jumla ya nyimbo nane,anazitaja baadhi ambazo tayari zinafanya vyema kwenye vituo mbalimbali vya redio kama vile Nenda,Utanikumbuka,tatizo umaskini pamoja na singali yake mpya aliyoitambulisha leo ndani ya kipindi cha Leo Tena iitwayo That Day.Vumi ambaye pia ni moja ya wasanii waliopikwa vyema na kituo cha THT kwa sasa yupo kwenye bendi ya Kimondo Sound a.k.a Kibajaji akijiendeleza zaidi.
Mtangazaji mwalikwa kwenye kipindi cha Leo Tena (kwenye chachandu la leo) aitwaye Husna B akitokea redio ya Coconut FM 88.2 a.k.a Mambo ya zenji,Zanzibar
Mtangazaji wa kipindi cha Leo Tena,Dina Marious kupitia redio ya Clouds FM 88.4 akifanya mahojiano mafupi na msanii wa muziki wa kizazi kipya aitwaye vumi ambaye kwa sasa yupo ndani ya bendi ya muziki wa dansii ya Kimondo Sound a.k.a Wanakibajaji ikiongozwa na Richard Mangustino aliyewahi kuwika miaka ya nyuma kwenye bendi kadhaa ikiwemo ya Diamond Sound enzi zilee za Ikibonda Nkoi.-Mashujaa Musica kuwasha Moto
-Watoto kucheza kiduku
-Vimwana wa Mashujaa kupamba jukwaa
Bendi ya Mashujaa Musica (Watoto wa Cash Lady) siku ya jumapili itashuka katika viwanja vya Nyama Chabezi Tegeta kutumbuiza wakati wa Bonanza litakaloshirikisha vikundi mbalimbali vya Viduku, na Michezo ya watoto ikiwa ni pamoja na Pool, kuvuta kamba michezo yote itaanza saa nane mchana ikiwa ni pamoja na michezo ya watoto ya kukimbiza Kuku na watoto kushindana kucheza makirikiti.
Burudani hiyo itaanza saa nane mchana ambapo Mashujaa Musica watatumbuiza chini ya wanamuziki wake wote akiwemo Rapa Mahili Ibrahim Milinda Nyeusi(Vuvuzela), Kiongozi wa Bendi Jado Fidifosi, Mtalaam wa Masauti Pasia Budance na Raja Rada.
Kwa mujibu wa msemaji wa Mashujaa musica, Shaaban Mpalule, Maandalizi yote kwa ajili ya onyesho hilo yamekamilika
“sisi tumeshajipanga kwa ajili ya burudani hiyo, hivyo kazi imebaki kwa wakazi wa eneo hilo kujitokeza kwa wingi ili washuhudie kazi mpya ya bendi yangu ikiwa ni pamoja na kupata radha mpya ya nyimbo mpya”alisema Mpalule
Hiyo itakuwa ni mara ya kwanza kwa bendi ya Mashujaa kutumbuiza katika eneo la ukunda wa Mbezi ambapo wamesema wataonyesha miondoko mbalimbali ikiwemo kuchinja bata, Wamefulia, kwa kiingilio cha shilingi elfu tatu wakubwa na watoto shilingi mia tano.
Wakazi wa Tegeta na maeneo yanayokaribiana mmetakiwa kufika siku hiyo ili kushuhudia burudani hizo, ambapo zawadi mbalimbali zimeandaliwa kwa mashabiki 50 wa kwanza watakaowahi kuingia kukaa katika sehemu zao.
Mashujaa Musica kwa sasa imekamilisha kurekodi nyimbo sita ambapo wanatazamia kufanya uzinduzi wa Album yao ya kwanza yenye nyimbo Mwanike, Moshi wa Sigara, Safari ya Vikwazo, Deodata, Mama Mi Nashangaa, sambamba na Intro ambazo zinaendelea kutesa katika sehemu mbalimbali za vyombo vya habari, Radio, Magazeti, na Tv.
Ratiba ya wiki Mashujaa Musica
Jumatano –Mashujaa Pub Vingunguti Kiingilio Kinywaji
Ijumaa - woodland kiwalani kwa jimmy kiingilio 3000
Jumamosi –Mashujaa Pub Vingunguti Kiingilio shilingi elfu 2000
Jumapili - Nyama Chabez Tegeta Kiingilio Shilingi 3000 wakubwa na watoto 500.


Pichani ni Washiriki wa Miss Temeke ambao nao walipewa nafasi ya kujinadi mbele ya wageni waalikwa waliofika kwenye shindano la Redds Miss Ilala lililofanyika mwishoni mwa wiki pale Ubungo Plaza.Shindano la kumsaka mlimbwende atakayelinyakua taji la Miss Temeke 2010 linalotarajia kufanyika pale TCC Sigara Chang'ombe Julai 9/ 2010, ambapo burudani itatolewa na kijana mahiri katika muziki wa bongofleva Banana Zorro na bendi yake ya B. Band.
Wanafunzi wa Chuo cha Ardhi walioshiriki mashindano ya Zain Africa Challenge (ZAC) wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kukabidhiwa vitita vyao leo asubuhi,makao makuu ya Zain,kutoka kulia ni Justine Rwerengera, Delphinus Kalumuna, Rodnique Sakaya na Justine Mwakalinga.
Wanafunzi wa Chuo Kuu cha Ardhi wakipokea kikombe cha ushiriki mashindano ya Zain Africa Challenge (ZAC) kutoka kwa Meneja Uhusiano wa Zain Tanzania Muganyizi Mutta.
Meneja Mahusiano wa Kampuni ya Zain Bw. Muganyizi Mutta, (kulia) akimkabidhi Mratibu wa Chuo Kikuu Huria Bw. Salim Hamad, dola 1600 kwa ajili ya kutambua ushiriki wao katika mashindano ya Zain Afrika Challenge Dar es saam, jana.Zain imekabidhi zawadi ya pesa taslim kwa Vyuo viliyoshiriki ZAC.
Diamond
Juma Nature
Kala Pina -Kikosi cha Mizinga
Joe Makini
Chege.
Offside Trick
Fid Q
Hussein Machozi
Godzilla
Mh Themba
Wadau Msimu wa tamasha la Fiesta 2010 linakaribia kuanza,na kama ujuavyo tamasha hilo husheheni mambo kibao kwa wapenzi/washabiki wao.safari hii kwa mara ya kwanza tena linagonga hodi ndani ya mji kasoro bahari,Morogoro.Wakazi wa Morogoro Fiesta hiyo 2010 inawajia mkoani mwenu ikiwa na kauli mbiu yake JIPANGUSE Rrrrrrrhhhhhhaaaaa..! Huku Mdhamini mkuu wa tamasha hio ambalo hufanyika mara moja kwa mwaka ni kampuni ya bia ya Serengeti Breweries Ltd.
Mdau mwanaharakati Peter Kazaula (kulia) akikabidhi mashine ya kuchuja maji aliyoitoa kwa hospitali kuu ya mkoa wa Kagera yenye thamani ya zaidi milioni 8 yenye uwezio wa kuchuja lita 6,500 kwa siku ambayo haitumii aina yoyote ya nishati. Anayepokea ni Kaimu Mganga Mfawidhi wa hospitali ya mkoa Dr Amri Byalugaba na kushoto ni mwenyekiti wa bodi ya hospitali ya mkoa Johansen Rutabingwa. Picha na Audax Mutiganzi wa Globu ya Jamii, Bukoba
