Monday, June 28, 2010

washindi wa Zain Africa Challenge wakabidhiwa zawadi zao leo

Wanafunzi wa Chuo cha Ardhi walioshiriki mashindano ya Zain Africa Challenge (ZAC) wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kukabidhiwa vitita vyao leo asubuhi,makao makuu ya Zain,kutoka kulia ni Justine Rwerengera, Delphinus Kalumuna, Rodnique Sakaya na Justine Mwakalinga.

Wanafunzi wa Chuo Kuu cha Ardhi wakipokea kikombe cha ushiriki mashindano ya Zain Africa Challenge (ZAC) kutoka kwa Meneja Uhusiano wa Zain Tanzania Muganyizi Mutta.

Meneja Mahusiano wa Kampuni ya Zain Bw. Muganyizi Mutta, (kulia) akimkabidhi Mratibu wa Chuo Kikuu Huria Bw. Salim Hamad, dola 1600 kwa ajili ya kutambua ushiriki wao katika mashindano ya Zain Afrika Challenge Dar es saam, jana.Zain imekabidhi zawadi ya pesa taslim kwa Vyuo viliyoshiriki ZAC.

Meneja Mahusiano wa Kampuni ya Zain Bw. Muganyizi Mutta, (kulia) akimkabidhi Mratibu wa Chuo Kikuu ARDHI Dr. Mbura Omari dola 1600 kwa ajili ya kutambua ushiriki wao katika mashindano ya Zain Afrika Challenge Dar es saam.

Kuna Maoni 0 mpaka sasa.