nimejifunza mengi Big Brother Africa Revolution-Elizabeth

Thursday, November 12, 2009
Mtangazaji wa Clouds Fm Jimmy Jamal akifanya mahojiano mafupi na aliyekuwa mshiriki wa Big Brother Africa Revolution Elizabeth Gupta mapema leo jijini Dar
Pichani kushoto ni Afisa huduma wa kampuni ya Multchoice Bi.Grace Urassa kati ni Aliyekuwa mshiriki wa Big Brother Africa Revolution Elizabeth Gupta pamoja na Meneja Huduma wa Multchoice Ronald Shelukindo walipokuwa wakizunguza na waandishi wa habari mapema leo jijini Dar.
Aliyekuwa mshiriki wa Big Brother Africa Revolution Elizabeth Gupta (pichani kati) akizungumza na waandishi wa habari mapema leo mchana kwenye Hoteli ya Paradise City jijini Dar, Elizabeth alirejea jana kutoka Afrika Kusini baada ya kuishi katika jumba hilo kwa siku 63 na baadaye kupigiwa kura ya kutoka nje na washiriki wa shindano hilo pamoja na mashabiki.
Aidha katika mkutano huo na waandishi wa habari,Elizabeth ameshukuru kwa kupata nafasi ya kushiriki shindano hilo,kwani anakiri wazi kuwa amejifunza mambo mengi na amepata mafanikio mengine mengi kutokana na ushiriki wake katika shindano la Big Brother Africa Revolution na anaamini kuwa wasichana wengi watakuwa wamejifunza mengi kupitia kwake, pia ameomba radhi kwa mashabiki ambao aliwakosea kwa namna moja ama nyingine katika maisha ya kila siku kwenye jumba hilo ambalo haikuwa rahisi kumfurahisha kila mmoja.
 
Muandishi: MICHUZI JR Tarehe: Thursday, November 12, 2009 | | Permalink |

Maoni: 0



Idadi ya watu